Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2021

MAMBO YA KUSHANGAZA KUHUSU KIFO.

Picha
MAMBO YA KUSHANGAZA KUHUSU KIFO. Kifo limekuwa jambo lenye kuogopwa na wengi kiasi kwamba siku hizi imekuwa nadra sana kuzungumziwa na watu, lengo lao likiwa ni kujifariji na kujisahaulisha kuwa siku moja watakufa. Hali hii imepewa jina kitaalamu inaitwa 'Thanatophobia' neno lenye maana "hofu ya kifo." Watalamu wa mambo ya saikolojia wamebainisha kuwa kwa kawaida kimtishacho binadamu ni kile asichokijua (Fear of the unknown), hali hii pia inaitwa Xenophobia. Hivyo wengi hukiogopa kifo kwa sababu hawakijui. Kuufahamu ukweli kuhusu kifo kutakusaidia kuendelea kuwa jasiri na kukuondolea hofu iliyojengeka ndani yetu kuhusu hatma ya kila mmoja wetu. KIFO NI NINI? Kuna nadharia nyingi sana kuhusu kifo. Nyingi kati ya nadharia hizo zimejikita zaidi katika masuala ya kidini na kiimani. Taarifa tulizonazo kisayansi kuhusu kifo ni kidogo sana hivi kwamba maswali yaliyopo ni mengi kuliko majibu. Kitabu Reasoning From The Scriptures kinaeleza kuwa kifo, "ni kukoma kwa ...

ZIFAHAMU SABABU, AINA NA DALILI ZA DEGEDEGE KWA WATOTO (SEIZURES)

Picha
 ZIFAHAMU SABABU, AINA NA DALILI ZA DEGEDEGE KWA WATOTO (SEIZURES) Degedege ni mojawapo ya matatizo hatari sana kwa watoto na huogopesha sana wazazi na walezi wengi. Katika hili kuna dhana tofauti tofauti zilizojengeka miongoni mwa wanajamii, ambapo baadhi huamini degedege ina uhusiano na mambo ya ushirikina na kwamba huweza kutibiwa kwa njia za namna hiyo. Wazazi na walezi wenye imani za namna hii hukataa kuwapeleka watoto wao hospitali wakiamini kuwa watakufa iwapo wataachwa wapate matibabu ya hospitali. Dhana nyingine iliyojengeka ni ile ya kuwa degedege ni tatizo linalotokea mara moja tu maishani mwa mtoto kitu ambacho si kweli. Aidha wapo pia baadhi ya wanajamii wanaohusisha degedege na ugonjwa wa Malaria pekee. Ukweli ni kwamba karibu asilimia 3 ya watoto chini ya miaka 15 hupata degedege, nusu ya hawa hupata degedege linalosababishwa na homa kali. Kwa maana hiyo basi, degedege pia linaweza kumpata mtoto asiye na homa kama kifafa. Inakadiriwa kuwa mtoto 1 kati ya 100 hup...

UMUHIMU WA AMANI

Picha
 AMANI Kamusi elezo ya mtandaoni Wikipedia, inaeleza kwamba "amani ni hali ya raha na usalama bila ugomvi; au kwa maneno mengine amani ni kinyume cha fujo au vita." Ni ndoto ya kila mtu kuishi maisha yenye amani na furaha. Karibia kila kitu tunachokifanya ni kwa sababu tunahitaji amani. Tunatamani mambo yote kutia ndani ndoa zetu zingedumu kwenye amani lakini wapi! Mataifa yanahaha kuisaka amani kwa mtutu wa bunduki. Wenye hekima na vitabu vingi vinavyoheshimika wamethibitisha thamani iliyopo katika amani, mathalani Biblia takatifu kwenye kitabu cha Methali Sura 17 mstari wa kwanza inasema "Ni afadhali kipande kikavu cha mkate mahali penye amani, Kuliko nyumba iliyojaa karamu pamoja na ugomvi."  Historia ya mwanadamu inaonyesha jitihada kubwa ambazo binadamu amezifanya kwa miaka mingi kuitafuta amani, kwa mfano baada ya vita vya kwanza vya ulimwengu vilivyopiganwa 1914 hadi 1918 kuisha, mapema mwaka 1919 mataifa washindi kwenye vita hiyo walianzisha Shirikisho la Ma...